Ijumaa, 18 Novemba 2016

SOMA HISTORIA ZA MASTAA TOKA MAREKANI KABLA YA KUWA MASTAA,FAMILIA ZAO,NA SASA NI MASTAA.HUWEZI AMINI WALIKOTOKA.

             


                              

                        UNDERTAKER 


   
   Kama wewe utakuwa ni
 mfuatiliaji mzuri wa mieleka ,Jina Undertaker Halitakuwa geni masikioni mwako,kwani mmoja kati ya wachezaji tishio katika  industry ya Mieleka ,(wrestling)


Undetaker anavyokuja
Kutokana na ujio wake Ulingoni mara Taa huzimika ghafla, zinapowashwa mara mtu yuko ndani ya Ulingo simchezo,sifa yake kubwa Huwa si muongeaji bali ni mtu wa Vitendo,amekuwa akifanya vizuri karibu Mapambano yake yote.


Mara Undertaker Ulingoni  

Undertaker ni nani basi.(Ni mchezaji Mieleka wa kimarekani)na hilo ni  jina lake bandia la(ulingoni)

Undertaker kono la Chuma

   Undertaker jina lake halisi ni Mark Wiliam Calaway.kazaliwa 24 march 1965 Houston ,Texas Inchini Marekani.
Wazazi wake Baba ni bwana Frank Compton Calaway,na mama ni Betty Truby Catherine.


   Elimu yake ya secondary kaipatia katika shule  ya secondary Waltrip High school ambapo huko alikuwa member katika timu ya mpira wa rugby(america football)na Basketball.
Undertaker akicheza Basketball akiwa high school mwenye namba 33 kifuani kushoto.
Ila alifanikiwa kugraduate 1983 na kisha kujiunga na chuo cha Angelina college,katika mji wa Lufkin texas on basketball scholarship.
  Mwaka 1985 alisajiriwa kwenye chuo cha Texas Wesleyan University ndani ya mji wa Fort Worth miongoni mwa miji mikubwa katika jimbo la Texas akichezea timu ya basketball,alikuwa mtu muhimu kwenye sport management, Alicheza  nafasi ya kati kama mtu mwenye nguvu ,mrefu na mwenye uzito kamili Big man ni mtu muhimu mwenye sifa kati ya moja ya nafasi tano muhimu kwenye mchezo wa basketball toka mwaka 1985 mpaka 1986.


Undertaker in Basketball team.

  Ila ilipofika mwaka 1986 Undertaker aliachana na chuo na kujikita zaidi kwenye michezo ,Ukweli alipenda  sana kuwa profession basketball(mchezaji basketball) huko uraya ,kabla hajamua na kubadili fikra zake  na kujikita katika mchezo wa mieleka(professional  wrestling) mwalimu wake wa mieleka alikuwa ni Don Jardine.

KATIKA MICHEZO YA MIELEKA


Undertaker kulia na Cane kushoto..
  Undertaker aliingia kwa mara ya kwanza ulingoni kwenye (WCCW)World Class Championship Wrestling)akitumia jina la  Texas Red, ila alipoteza mechi hiyo alipopambana na Bruiser Brody.hatimaye mwaka 1988 baada ya miaka minne ya Promotion,Alitoka huko na kujiunga na Coninental Wrestling Association,ambapo alikuja kuwa sehemu ya United Wrestling.
UNDERTAKER ALIYESIMAMA KWENYE HELL IN THE CAGE

Jumatano, 16 Novemba 2016

FUNGUKA KUPITIA HISTORIA ZA MAISHA YA MASTAA KUTOKA CHINA.KABLA YA KUWA MASTAA NA VIPI WALIVYOKUJA KUFANIKIWA ,NA FAMILIA ZAO KWA UJUMLA


     
      HISTORIA YA JACK CHAIN.

MCHEZAJI MAHIRI WA MICHEZO YA KARATE ,NA STLYE ZINGINE ZA MAPIGANO,NA  MWENYE VIPAJI VINGI PAMOJA NA UIGIZAJI,ACROBATIC,NA HATA UIMBAJI.


 


  Jack chain kazaliwa  7 April 1954 katika eneo liliofahamika kama British Hong Kong kipindi cha ukoloni . Jina lake halisi ni Chan Kong Sang , Bali jack ni  jina la usanii tu ama jina katika fani yake ya uigizaji.

JACK KWENYE POSE KALI LA MAPIGANO.
Baba yake ni Charles chan na Mama Lee Lee Chain refugee from the Chinese Civil War. kabla ya kubadili kazi bwana Charles chan .Jack akiwa mdogo alibatizwa jina la utani kama pao pao yaani kitenesi (cannonball)  kutokana na wepesi wake wa kuruka ruka .

JACK CHAIN IKIMPA MAFUNZO JADEN SMITH MTOTO WA WILL SMITH KWENYE KARATE KIDS

JACK AKIMNOA JADEN SMITH KWENYE KARATE KIDS

      Jack alianza masomo yake ya awali, katika shule ya msingi ya Nah- Nhwa  kisiwani HongKong Hata hivyo alifeli kwa mwaka wake wa kwanza. wakati huo Wazazi wake walikuwa wafanya kazi katika balozi ya Ufaransa ndani ya jiji la Hong Kong .na Jack alikulia pembezoni mwa wilaya ya Victoria Peak consul’s redendence ndani mji huo wa Hong Kong.
  Ila hatimae mwaka (1960)wazazi walihama  na kelekea katika mji Canberra inchini Australia,ambapo baba yake alikwenda kufanya kazi, kama mpishi mkuu katika balozi ya Marekani,Hivyo Jack alipelekwa nchini China kusoma katika chuo cha sanaa ya maigizo na michezo.A Perking Opera School .(Drama Acamemy)
    chini ya  Master Yu Jim –yuen. Jack alichukua mafunzo kwa miaka 10. katika martial arts na Acrobatics  (sarakasi na mapigano). 



KUTOKA KUSHOTO YUEN BIAO KATI SAMO HUNG NA KULIA JACK CHAIN

  Na hapo ndio alipopata nafasi ya kuingia katika Seven little   Fortune (saba wenye bahatijina lake la kisanii alifamika kama Yuen Lo kwa wakati huo, ambalo hilo lilikuwa ni jina la master wake.aliungana na marafiki wawili vipenzi amabyo baadaye walikuja kujulikana kama (Three brothers ama three Dragons, Sammo Hung na Yuen Biao.)  


kutoka kushoto ni Jack kati ni Samo hung na kulia ni Yuen Biao

  NI NANI ALIMBATIZA JINA LA  (JACK)
   Mwaka 1976 Jack alirudi Australia kwa wazazi wake na kujiunga chuo cha Dickson ama (Dickson College) na kufanya kazi za ujenzi (Mmoja wa mafundi (costruction worker)  aliyetambulika kwa jina moja la Jack,Ndie aliyembatiza jina hilo la utani.kwani alishindwa kutamka jina lake halisi kwa kichina yaani Chan Kong Sang.hatimaye akajikuta kapewa jina jack badala yake.au a little Jack  (jack mdogo) ama Jackie,aliendelea kulitumia jina hilo kwa kipindi kirefu ,mpaka alipokuja kulibadili mwishoni mwa 1990 na kuitwa jina lake la ukoo (Fong Si –Lung).Ambalo ndilo likuwa jina upande wa ukoo wa baba yake.


  NI WAPI ALICHUKUA MAFUNZO           ZAIDI YA MAPIGANO.



JACK KATIKA POSE LA SNAKE

  Baada ya kuingia katika industry filamu Jack na sammo Hung waliapata nafasi ya kuchukua mafunzo ya Hapkido chini ya master Jin Pal Kim. hatimaye Jack akapata mkanda mweusi (black belt).
Aliendelea kujifunza style zingine za mapigano zaidi za Martial arts kama vile Karate,judo,taekondo na Jeet Kune Do.
      Baada ya kuingia katika industry filamu Jack na sammo Hung waliapata nafasi ya kuchukua mafunzo ya Hapkido chini ya master Jin Pal Kim. hatimaye Jack akapata mkanda mweusi (black belt).
Aliendelea kujifunza style zingine za mapigano zaidi za Martial arts kama vile Karate,judo,taekondo na Jeet Kune Do.


JACK CHAIN AKICHUKUA MAFUNZO
  
                    LINI ALIANZA KUGIZA?

    Alianza kuigiza tangu akiwa mdogo na kutokea katika scene chache tangu akiwa na umri wa miaka 5 .Ila alipofikisha umri wa miakaalionekana  kwenye little Fortune katika filamu ya Big an Little Wong Tin  Bar (1962)akiigiza na mwanadada Li li Hua kama mama yake,Na hata hivyo alitokea tena na mwanadada katika filamu The Love Eterne (1963)Pamoja na part mbalimbali za filamu ,katika KING HU’S mwaka 1966 ya Come drink with me. Baada ya kutokea katika filamu kadha za Kung fu ikiwemo  ya A touch of Zen,ndipo aliposaini na Chu Mu;s Great Earth Film Company ,akiwa na umri wa miaka 17.Na kuanza kufanya kazi kama Stuntman (michezo ya Hatari) kwenye filamu aliyocheza na Bruce lee ya Fist of Furry na Enter the Dragon akitumia jina la kisani kama Chan Yuen Lung.




  Hapo Ndipo alipopata nafasi kwa mara kwanza kuigiza kama muigizaji nyota ( movie  star)katika filamu ya Little Tiger of Canton ambapo ilizuiwa kutolewa 1973 na hatimaye ikaruhusiwa mwaka 1978 .ilikuwa ni filamu kali,ambapo jack alicheza kama kijana alikuja kulipiza kisasi juu ya kifo cha baba yake akitokea kwenye kundi la siri la uharifu huko inchini china.
   Kutokana upungufu wa fedha za kuwekeza katika filamu na michezo ya stunt 1975 kuyumba. Jack aliamua kuingia kwenye filamu za Comedic pamoja na Adult film,Ikiwemo All in the Family,na hii ndio ilikuwa filamu yake ya kwanza kuigiza utupu na pia filamu yake ya kwanza kuigiza bila ya scene ya mapigano wala michezo ya stunt. Na hata hivyo Jack akatokea tena katika sex scene ya Shinjuku Incident

 JACK CHAIN NA MUZIKI AKIPERFOM


JACK CHAIN AKIIMBA 


 Mbali na uigizaji jack ni mwanamuziki, Na keshatoa records mbalimbali,Akiwa mdogo alikuwa akihudhuria Mafunzo ya kuimba, The Peking Opera school.Alianza kuimba toka mwaka 1980, na kumfanya kuwa ni mwanmuziki mwenye mafanikio makubwa huko Hong na Asia. 
  Amekwisha toa Album takrbani 20 toka mwaka 1984.Amekuwa akiimba katika lugha tofauti KIJAPANI,Mandarini, Cantonees ,Kitaiwaini na Kingeleza.
Karibu filamu zake zote Sauti za nyimbo zinazosikika mwisho wakati picha inaisha ni nyimbo alizoimba Jack chain.
Wimbo wake wa kwanza ulikuwa ni ‘kung Fu fighting man”wimbo huu utausikia katika filamu ya The Young Master (1980) mwishoni wakati maandishi yapanda kuonyesha washiriki wa filamu.Karibu ya record zake 10 zimekuwa zikitumika kama soundtrack album za filamu zake.

Wimbo wake aliouimba katika lugha ya Cantones story of hero unaweza kuusikia katika filamu ya police story, na ulichaguliwa na Royal Hong Kong Police na kuuingiza katika Idara yao ya Matangazo 1984. HEBU FUATILIA UJUE MENGI USIOYAJUA KUHUSU JACK NA FAMILIA YAKE .inaendeleaa........



JACK CHAIN KUSHOTO NA MWANAYE WA KWANZA KULIA
JAYCEE CHAIN





                            BRUCE LEE 
                                                                MTAALAMU WA MCHEZO WA KUNGFU KATIKA STLYE YA  TAEKUDO
                        BRUCE LEE
HISTORIA YA MAISHA YAKE FAMILIA NA ALIPOTOKA HADI KUJA KUWA THE                                    WORLD SUPER STAR.

Bruce Lee kalizaliwa 27/11/1940 Chinatown ,Sanfrancisco,Califonia Inchini Marekani.
Bruce na kulia na mkewe Linda Lee Cadwell
 Alimuo bibie Linda Lee Cadwell 1964 ambaye alikuwa mwalimu wa Kimarekani(american teacher)
Brando Lee akichukua mafunzo kutoka kwa baba yake
Mafunzo yakiendelea
hapa ndipo unapokamilika usemi wa mtoto wa nyoka ni nyoka.

Bruce lee kushoto  brando lee kati  Mkewe kulia Enzi Hizo.


Bruce mkewe na waoto wawili
Wawili hawa walibahatika kupata watoto wawili wa kwanza ni wakiume ambaye ni Brandon Lee na wapili ni wakike Shanon Lee.

Bruce Lee na wanaye Brandon lee kushoto  kulia Shanon Lee enzi za uhai.
   Utakubaliana nami kuwa Bruce lee alikuwa ni moto wa kuotea mbali...


Bruce In action
..enzi Hizo Hakuna aliweza Kumuondoa kwenye nafasi yake katika mapambano mbalimbali na hata hivyo hakuna alifanikiwa kuziba pengo lake mpaka sasa, ingawaje wapo wengi wanaofanya vizuri.


Aliyekaa ni IP MAN ni Mwalimu wa Bruce na aliyesimama ni Bruce Lee.
YIP MAN (IP MAN) ndiye mwalimu wa Bruce Lee ,Master huyu kazaliwa 1 octoba 1893 ,Master YIP MAN alikuwa akifundisha WING CHUN.Wing Chun ni style za mapigano ya Martial arts iliyobuniwa huko China kusini (southern China)miaka 300 iliyopita.Master IP Alifundisha wanafunzi wengi ambao wengi wao walikuja kuwa ma Master. Miongoni mwao ni Bruce Lee na wengine,Ila hatimaye master wake  Alifariki dunia 2 desemba 1972.Hata hivyo Bruce naye alibeba mikoba ya master na akaendelea kufundisha,hawa ni baadhi ya wanafunzi ambayo aliwahi kuwafundisha.

BRUCE NA CHUCK NORRIS
 Style hizi za mapigano hasa ya Jeet kune do,ni pamoja na Joe Lewis,Mike Stone,na chuck Norris,


Joe Lewis mwanafunzi wa Bruce
Mike stone mwanafunzi wa Bruce Lee 
Chuck Norris mwanafunzi wa Bruce
Baadhi yao walifanikiwa kushinda mikanda na medani mbalimbali walipokwenda kucheza katika mashindano ya karate,mojawapo ni  Us Karate Championship 1968 Joe Lewis alishinda.


Joe Lewis kulia akiwa na washindi wengine.
 Miongoni mwa wanafunzi waliokuja kuwa mastaa na kufanya vizuri ni chuck Norris,Joe lewis hata filamu nyingi walizocheza walifanya vizuri na miongoni mwao walifungua vyuo vya karate huko inchini Marekani.
picha ya pamoja bruce kulia wapili toka kulia coburn,wa kwanza kutoka kushoto mike stone na wapili toka kushoto chuki Noris 

Katika Hospital ilikothibishwa kifo chake
Bruce Lee alindondoka kipindi wakishuti Enter The Dragon, in Golden Havest in Hong.alikua akisumbuliwa na kizungungu na maumivu ya kichwa,mara tu alipodondoka alikimbizwa katika hospital ya baptist Katika Jiji la Hong Kong kwenye kitongoji cha Kowloon Tong.


Bruce Lee Ndani ya Geneza Tayari akiagawa.
 ambapo madaktari waligundua kuwa Alikuwa na tatizo la  (Cerebral edema),Uvimbe kwenye Ubongo.Ingwaje jitihada zilifanywa kuokoa maisha yake hatimaye alifariki 20 julai mwaka 1973 akiwa na Umri miaka 32.


BRUCE LEE NA BOLO YOUNG
Hizi ni baadhi ya filamu kali alizofanya enzi za uhai wake .The Big Boss(1971)



Fist of Fury (1972) Golden Harvest way Of Dragoni(1972)



Na alizikwa 31 julai 1973 katika makaburi ya Lakeview settle ,Washngton Dc,Huko nchini marekani.



Makaburi  ya Baba na Mtoto .Bruce Lee kushoto na kulia Brandon Ingawaje alifariki ila aliacha watoto wawili nao walikuwa Moto wa kuotea mbali Shanon Lee na Brandon Lee. walifuata nyayo Zile zile za Bruce Lee,Ila bahati mbaya 13 machi 1993 Brando lee naye aliaga dunia.Shanon Lee na mama yake ndio waliobaki na kuendeleza chuo alichofungua Bruce Lee huko nchini marekani .


Brandon Lee na Shanon Lee
watoto wa bruce lee.